Jumamosi, 11 Machi 2017

Kinachorndelea ndani ya ccm

KWA UFUPI:

Machi 11, 2017 - Dodoma

Habari kutoka Makao Makuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Dodoma ambapo Mkutano Mkuu unaendelea ni kwamba, baadhi ya wananchama wa CCM wamevuliwa uanachama huku wengine wakipewa onyo kali kwa sababu mbalimbali, kubwa ikiwa ni usaliti katika uchaguzi mkuu mwaka 2015.

Miongoni wa waliofukuzwa uanachama ni pamoja na mwanachama mkongwe na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake (UWT) Sophia Simba huku Adam Kimbisa akisamehewa na Emmanuel Nchimbi akipewa onyo kali. Onyo kali alilopewa Nchimbi ina maana kuwa hatoruhusiwa kugombea nafasi yoyote kwa miaka minne.

Kufuatia maamuzi hayo, Sophia Simba amepoteza rasmi nafasi yake ya Ubunge wa Viti maalumu na Uenyekiti wa UWT kwani nafasi hizo zinahitaji mtu ambaye ni mwanachama wa chama aweze kuzishika. Hivyo, CCM italazimika kupeleka jina jingine Tume ya Uchaguzi kuteua mbunge wa kuziba nafasi ya Sophia, huku nafasi yake ya Uenyekiti UWT ikisubiri uchaguzi baadae mwaka huu.

Wengine waliovuliwa uanachama ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni Madenge, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilala, Assa Simba, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Christopher Sanya, Mwenyekiti Mkoa wa Shinyanga Ernest Kwirasa, Mwenyekiti wa Mkoa wa Iringa, Nesta Msabatavangu, Mjumbe wa Halamshauri Kuu (NEC) ya CCM, Ali Sumaye, Mjumbe wa NEC Arumeru, Mathias Manga.

Pia, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Longido, Leizer amefukuzwa uanachama pamoja na Mwenyekiti wa CCM Arusha Mjini, Saileli Mollel, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Gairo, Omary Awadhi, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Muleba, Mwenyekiti wa CCM Babati, Mwenyekiti wa CCM Wilaya Bunda, Mjumbe wa NEC Gureta.

Waliopewa onyo kali kwa makosa mbalimbali ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Iringa Mjini, Ahmed Kiponza ambaye amepewa onyo kali na kuondolewa madarakani, Mjumbe wa NEC Mkoa wa Singida, Hassa Mzaha, Mwenyekiti wa UWT Gezabulu, Mjumbe wa NEC Kilwa, Ali Mchumo na Mjumbe wa NEC Tunduru, Cheif Kalolo ambaye amevuliwa ujumbe huo na kupewa onyo kali.

Recodi ya zanaco kuelekea mechi ya leo

Kikosi cha yanga kitakachocheza mechibya leo

YOUNG AFRICAN LINE UP AGAIST ZANACO FC
1 Deogratius Munishi
2 Hassan Kessy
3 Hajy Mwinyi
4 Nadir Haroub
5 Vincent Bossou
6 Kelvin Yondan
7 Simon Msuva
8 Justine Zullu
9 Donald Ngoma
10 Thaban Kamusoko
11 Obrey Chirwa
AKIBA
Ali mustaph
Oscar joshua
Juma Abdul
Imanuel martin
Juma mahadhi
Deusi kaseke

Tengeneza mil 5 kwa kilimo cha mahindi

MAKALA FUPI YA KILIMO CHA ZAO LA MAHINDI (CORN).
Imeandaliwa na Agronomist. Boniphace.

MAHINDI (CORN).
Ni zao linalolimwa maeneo mbalimbali yenye ardhi ya uchachu kiasi pamoja na chumvi kiasi (pH 6.5 - 7.5).
MBEGU (SEEDS/ VARIETIES).
Kuna aina mbili za mbegu za Mahindi duniani.
1. Mbegu chotara / Hybrid seeds ( Seedco 627, PHD 3253, Syngenta 634, DK 8090 na KITALE).

2. Mbegu za kienyeji au Kukamua/ OPv seeds (STAHA, STUKA na TAN 250).

UANDAAJI WA SHAMBA LA MAHINDI.
Tutaanza kwa kukwatua na kuweka usawa wa ardhi kabla hujapiga mashimo.
Vipimo elekezi vya upandwaji wa mbegu ya mahindi ni 80 * 25cm yaani mstari kwa mstari ni sentimita 80 wakati shimo kwa shimo ni sentimita 25.

MATUMIZI (VIPIMO) SAHIHI YA MBOLEA KWENYE SHAMBA LA MAHINDI.
1. DAP
Kwenye hatua ya upandaji kitaalamu tunashauri upandie mbolea ya DAP au Samadi. Utapima gram 5 (kisoda kimoja kwa lugha ya shambani) kwa kila shimo.
Kwa faida ya mkulima mbegu ya mahindi huota ndani ya siku 3 mpaka 7 kulingana na aina ya udongo.
2. NPK
Baada ya siku 14 hadi 21 toka hindi lilipoota, unashauriwa kunyunyuzia mbolea ya NPK. Unaweza kwenda kwa gram 10 au 15 kwa shina ambazo ni sawa na visoda viwili au vitatu kwa lugha ya shambani.
3. CAN
Kulingana utofauti wa ukomavu wa mbegu tofauti za mahindi, zipo zile za mda mfupi (Early Maturity) pia zipo za mda mrefu (Late Maturity). Sasa uwekaji wa mbolea hii huwa hatuzingatii siku za tangia mmea kuota bali tunazingatia hatua ya mmea (Stage of the plant).
Kitaalamu tunashauri weka mbolea ya CAN kwa kufuata kipimo elekezi kwenye muhindi wako mara tu Mahindi yanapokaribia kuchanua au kutoa mbelewele (Tarselling stage). Kwa lugha ya kimaandishi tunasema unafanya "Second Top Dressing". Baada ya kufanya hvyo upande wa zoezi zima la mbolea utakuwa umemaliza na badala yake utakuwa unasubiria mavuno tu.

KUJIKINGA NA ATHARI ZA WADUDU KATIKA ZAO LA MAHINDI (VIATILIFU).
1. Karate 5 EC pamoja na 2. Match 5 EC.
Hizo zote ni sumu zitumikazo kuua na kuzuia athari za wadudu wanaotoboa na kukata Mahindi. Kama vile Viwavi jeshi, Ng'onyo na aina mbali mbali za wadudu jamii ya matobozi kwenye zao la Mahindi.
Vipimo: Utapima 20mls za Karate kwa maji ya bomba/solo la maji yenye ujazo ya Lita 20. Au
Match 25mls kwa maji ya bomba/solo la maji yenye ujazo ya Lita 20.
Kitaalamu tunashauri ewe mkulima upige sumu hizi, siku ya 14, 28 na 42 au 45 toka Mahindi yako yalipoota na sio toka ulipopanda.
3. Actara na mbadala wake waweza kuwa 4. Evisect.
Hii ni sumu inayoenda kuua wasambazaji (Vectors) wanaoenda kusambaza gonjwa la kirusi lifahamikalo kama " Maize Streak Virus" au kwa kifupi huita MSV.
Upimaji: Kwa Actara ambayo ndio sumu mama ya kutibu tatizo hili utatakiwa upime 8 gram kwa bomba/ solo la Lita 20 za maji.
Muda: Kitaalamu tunashauri upige sumu hii siku ya 28 tangia Mahindi yako yalipoota na sio tangia ulipopanda.

VIUA GUGU KWENYE ZAO LA MAHINDI (HERBICIDES)
Kwa swala hili sitotaka kuingia sana ndani zaidi ya kutaja viua gugu elekezi kwa maana mkulima atakayehitaji kufahamu zaidi itabidi awasiliane nami, kwa kuanza
1. Primagram gold
2. Dual Gold
3. Maguguma
4. Servian
5. Twigaquat
6. Rondopaz pamoja na
7. Muparaxon.

IDADI YA MBEGU, IDADI YA MIMEA NA MAVUNO KWA EKARI.
1. MBEGU.
Mbegu kilo 10 zatosha kwa shamba la ukubwa wa ekari 1.
2. IDADI YA MIMEA
Kwa shamba la ukubwa ekari moja unakadiriwa kuwa na jumla ya mimea 20000, Kitaalamu tunasema "Plant population per Acre is around 20000"
3. MAVUNO (YIELD PER ACRE).
Kulingana na mbegu uliyotumia, lakini kwa wastani makadilio huwa ni kati ya gunia 25 mpaka 35 kwa ekari. Cha msingi pendeni kutumia mbegu chotara na sio mbegu za kukamua.

Warioba:tuungane kutokomeza njaa.

Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema kutokana na upungufu wa chakula uliopo nchini, Serikali ijiandae katika kukabiliana na hali hiyo.

Pia, amewataka viongozi kuacha kubishana, badala yake waungane kutoa elimu kwa wananchi ya namna watakavyotumia mvua zinazonyesha kwa ajili ya kilimo cha mazao yanayovumilia ukame.

“Hivi sasa kuna dalili za upungufu wa chakula na hili ni tatizo, hivyo Serikali ijiandae. Tusianze kubishana kama kuna njaa au kuna upungufu wa chakula au huyu kasema hivi, yule kasema hivi kwa sababu mabishano hayo hayatawasaidia wananchi,” alisema Jaji Warioba jana wakati akizindua kitabu cha Mtandao wa Wanawake na Katiba.

Mbali na hilo, kiongozi huyo alisema kinachotakiwa kwa sasa ni jamii kupewa elimu na taarifa za hali ya hewa ili iweze kujua  hali halisi ya mvua na namna itakavyozitumia kwa kilimo.

Kuhusu mapambano ya dawa za kulevya, alisema hayapaswi kuwa ya mtu mmoja, bali Taifa zima liungane na viongozi wasione kama ni tukio la kawaida.

Jaji huyo mstaafu alisema viongozi wanapaswa kwenda kwa wananchi kuwapa elimu ili wajue madhara na namna ya kujiokoa na tatizo hilo kwa lengo la kulinda kizazi kilichopo na vile vinavyokuja. “Napenda tushirikiane kwa pamoja katika kuongeza nguvu kuzuia, kupambana na kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya pamoja na kuwasaidia wale ambao wamepata madhara kutokana na matumizi ya dawa hizo,” alisema